Friday, May 4, 2012

NYARAKA ZA OSAMA BIN LADEN KUCHAPISHWA LEO

Marekani imechapisha baadhi ya nyaraka zilizokamatwa kwenye maficho ya mwisho ya aliyekuwa kiongozi wa mtandao wa al Qaida, Osama bin Laden. Nyaraka hizo zinaionyesha al Qaida kama kundi lililozingirwa na kudhoofika.
Nyaraka hizo ambazo ziliwekwa kwenye mtandao Alhamisi, ni sehemu ndogo tu ya zile zilizogunduliwa na Marekani, baada ya wanajeshi wake kumvamia na kumuuwa Osama bin Laden nchini Pakistan mwaka uliopita. Wamefanya makusudi, kuonyesha upande mbaya sana wa al Qaida, kwa sababu kuuawa kwa bin Laden kunachukuliwa na utawala wa Rais Barack Obama kama tukio muhimu kwa usalama wa taifa. Tukio hilo pia ni mada inayopendelewa sana na Rais Obama katika kampeni yake ya kutaka kuchaguliwa tena.

No comments:

Post a Comment